CCM,Chadema jino kwa jino Ubunge Kinondoni.


Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Zanzibar, Salum ametangaza vita na chama cha Mapinduzi (CCM) katika uchaguzi wa Ubunge jimbo la Kinondoni.

Akizungumza baada ya kuchukua fomu Mwalimu amewataka wanachama wa chama hicho kuwa wavumilivu katika kipindi hiki cha muda mfupi.


Kwa hiyo baada ya muda huo kupita siku ya kesho bila ya shaka nitakuwa mgombea rasmi wa jimbo la Kinondoni ambaye nisiyekuwa na doa kwa ajili ya mapambano hayo  alisistiza Mhe. Salum Mwalimu.

Mwalimu amesisitiza kuwa safari hii hawakuja kubip katika kinyang’anyiro cha Ubunge Kinondoni kama ilivyojitokeza katika chaguzi nyingine za marudio zilizopita.

Tunamaanisha na tunaamini kabisa kama nidhamu ya siasa waliyoikataa, hapa watairudisha na wasipoikubali kuirudisha Kinondoni maana yake ustaarabu katika siasa tunaamini utakuwa umekwishamalizika. Hatutokuwa wa kulia, safarii hii ikibidi tutawasababisha wale waliosababisha sisi tunalialia wao ndio walie

Amesema Mwalimu Kuhusu dhamira yake ya kugombea Ubunge, Mwalimu amesema amedhamilia na amejitoa kusimamia haki ya wananchi wa Jimbo la Kinondoni na kuahidi hatoweza kuyumba

Comments