
Akizungumza na Zanzibar24 Mkurugenzi wa
Baraza la Manispaa Zanzibar Aboud Hassan Serenge amesema kwa mwaka 2018
watahakikisha sheria zote zilizopangwa kuimarisha mazingira kwa
upandaji wa bustani pamoja na udhibiti wa taka zinafanikiwa ili kulinda
mandhari ya nchi.
Serenge amesema mashirikiana baina ya
serikali wananchi na baraza hilo yanahitajika ili kufanikisha adhma ya
kuufanya mji wa Zanzibar kuwa na haiba nzuri hali itakayosaidia
kupunguza maradhi yanayoambukiza ikiwemo kipindupindu.
chanzo:Zanzibar24
Comments