SMS kuimarisha huduma za Afya.

Image result for haroun ali suleimanWaziri wa Nchi ofisi ya Rais Katiba ,Sheria ,Utumishi wa Ummana Utawala Bora Zanzibar Mhe Haroun Ali Suleiman amesema kwamba serikali ya Mapinduzi  ya Zanzibar itaendelea na dhamira yake yakutoa huduma za  afya  bure  kwa wananchi wake ,ikiwa ni utekelezaji  wa ahadi ya Mapinduzi  Matukufu ya mwaka 1964.

Mhe Haruon ameyasema  hayo leo huko katika viwanja vya Hospital ya Abdullah Mzee Mkoani  ikiwa ni sehemu ya shamra shamra za maadhimisho kutimia miaka 54 ya  Mapinduzi  matukufu ya zanzibar zilizoanza leo.

Amesema  sera za  Mapinduzi  ya mwaka 1964 imeahidi bayana kuwapatia wananchi wake  huduma muhimu za ayfa  bila ya malipo ,jambo ambalo linaendelezwa hadi sasa.

Mapema  Mhe Haroun amewasisitiza wananchi kudumisha suala la usafi   hususan katika maeneo  ya mahospital ,ili kulinda ayfa za wananchi.

Amesema suala la usafi ni muhimu kwa maisha ya mwanadamu,hivyo ni vyema  jambo hilo kuendelezwa.


Naye Kaimu Mkuu wa wa wilaya ya Mkoani ,ambaye pia ni mkuu wa wilaya ya chake chake Ndg Rashid Hadidi  Rashid amesema kuwa wilaya hiyo imejipanga vyakutosha kusimamia  suala la usafi katika maeneo mbali mbali wilayani humo ikiwa ni pamoja nakutoa mafunzo kwa wananchi juu ya udhibiti na usimamizi mzuri wa mazingira.

Comments