Jeshi la Polisi latoa tahadhari katika kipindi hichi cha skukuu kwa wananchi na madereva hasa hasa T-One.

alawitiJeshi la Polisi la Mkoa wa Mjini Magharib limewatahadharisha wananchi kutojihusisha  na uvunjifu wa amani katika kuelekea sherehe za Krismasi  na mwaka mpya.

Akizungumza na Waandishi wa Habari Kamanda Hassan Nassiri amesema Jeshi lipo imara  kuhakikisha linadhibiti  na kulinda amani  za wananchi pamoja na mali zao katika kipindi hichi cha sherehe za Krismasi na mwaka mpya.

Amesema mwananchi yeyote atakaejihusisha na matendo ya uvunjifu wa amani endapo watatiwa nguvuni na jeshi hilo  hatua kali watachukuliwa  dhidi yake.

Aidha Kamanda Nassir amewataka waendesha vyombo vya moto wanaojulikana kama T-One  kutoitumia fursa hiyo kwa kushangiria kwa fujo za kuendesha vyombo vyao kwa mwendo wa kasi katika  mizunguko ya  mikutano ya barabara kama Roundi ya bauti.

Hata hivyo amesema  ulinzi utaimarishwa katika makanisa yote yatakayofanyika ibada pamoja na viwanja vyote vitakavyotumika  katika kusherehekea skukuu hizo mbili.

Sambamba na hayo ametoa wito kwa jamii kuwacha tabia ya kuchora  barabara  katika kipindi hichi kwani hali ile inachafua miundombinu ya serikali.

chanzo: zanzibar24.

Comments