Iran yalaani mashambulizi ya anga ya Saudia dhidi ya soko, yaliyoua 70 Yemen.

Iran yalaani mashambulizi ya anga ya Saudia dhidi ya soko, yaliyoua 70 YemenMsemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amelaani mashambulizi ya anga yaliyofanywa na ndege za kivita za Saudi Arabia dhidi ya soko moja mkoani Taizz kusini maghribi mwa Yemen na kuua makumi ya watu.

Bahram Qassemi amesema ni jambo la kutamausha kuiona Saudia inalipiza kisasi kwa raia wasio na ulinzi, kutokana na kushindwa kwake katika medani za vita.

Amesema mashambulizi haya ya kiwendawazimu yanayofanywa na Saudia kwa kutumia silaha za Marekani ni ya kusikitisha na yanafanyika mbele ya kimya cha jamii ya kimataifa.

Kwa mujibu wa Wizara ya Afya ya Yemen, mashambulizi hayo ya anga ndani ya masaa 48 yaliyopita katika wilaya ya Heime nchini Yemen yamesababisha mauaji ya watu 71 huku wengine zaidi ya 100 wakijeruhiwa.

Msemaji wa harakati ya Ansarullah ya Yemen, Mohammad Abdulsalam amelaani hujuma hizo dhidi mkusanyiko mkubwa wa raia wasio na hatia sokoni na kusisitiza kuwa, hatua hiyo inaashiria kufeli kwa njama na matarajio ya Saudia huko Yemen.

Katika hatua nyingine, ndege za kijeshi za Saudia zimetekeleza mashambulizi ya anga dhidi ya makazi ya watu katika mkoa wa Hudaydah na kuua watu 14 wa familia moja.

chanzo: parstoday.

Comments