Gadi ya Pwani nchini Italia yaokoa mamia ya wahajiri katika bahari ya Mediterranea.

Gadi ya Pwani nchini Italia yaokoa mamia ya wahajiri katika bahari ya Mediterranea Askari wa Gadi ya Pwani ya Italia wametangaza habari ya kuwaokoa wahajiri 250 katika bahari ya Mediterranea.

Taarifa ya Gadi ya Pwani ya Italia imesema wahajiri hao waliokuwa kwenye boti moja ya mpira na mbili ndogo za plastiki wameokolewa katika operesheni zilizofanyika kati ya Jumatatu usiku na jana Jumanne.

Siku chache zilizopita, Kikosi cha Jeshi la Majini la Libya kiliokoa wahajiri karibu 200 katika pwani ya magharibi mwa nchi hiyo katika bahari ya Mediterania waliokuwa wakielekea Ulaya.

Libya imekuwa ikitumiwa kama nukta ya kuanzia safari za wakimbizi na wahajiri vijana wa Kiafrika kuelekea Ulaya.

Tangu mwanzoni mwa mwaka huu wa 2017 hadi sasa, karibu wakimbizi elfu tatu wameaga dunia wakijaribu kufika Ulaya kupitia Bahari ya Mediterania, vifo ambavyo vingi vimetokea katika njia ya bahari kutoka Libya kuelekea Italia. 

Mwaka uliopita, zaidi ya wahajiri elfu tano aghalabu yao wakiwa wa Kiafrika walipoteza maisha katika safari hizo hatari.

chanzo: parstoday.

Comments