Bunge la Uganda lajadili ukomo wa Urais kwa siku ya tatu.

Bunge la UgandaBunge la Uganda limeanza siku ya tatu za kujadili mswada utakao mruhusu Rais Yoweri Museveni kugombea kwa awamu ya sita.
Vurugu kati ya wabunge na vikosi vya usalama zilitokea jana wakati muswada huo ulipoanza kujadiliwa.
Mwandishi wa BBC Catherine Byrahunga anasema sasa nchi inasubiri kuona namna ambavyo wabunge hao watapiga kura katika swala hilo nyeti la kubadilisha katiba.
Mipango ya kutoa ukomo wa umri wa Rais umepelekea kuwa na maandamano nchini Uganda.
Wengi wanaona kama mpenyo wa Yoweri Museveni kuwa Rais wa maisha.
Wakati huo huo , wafuasi wake wanasema kuwa wanaweza kupigia kura ya kumtoa wakati wowote. Lakini wapinzani wanahisi kuwa uchaguzi nchini Uganda haujawahi kuwa huru na hautakuwa huru kwa siku za usoni.Wabunge wa Uganda wakipigana baada ya kuhitilafiana
Chanzo:BBc.

Comments