Wananchi wailalamikia SMZ ongezeko la baa karibu na makaazi ya watu

Wananchi wameiomba Serikali  ya Mapinduzi Zanzibar kuziondoa baa zote zilizojengwa karibu na makaazi ya wananchi  ili kunusuru vizazi visiweze kupotea  pamoja na kunusuru afya za wananchi.

Wakizungumza na Zanzibar24  Baadhi wa Wananchi wa kilimani,Amani Fresha na Migomban  wamesema kila mwaka hufika katika mahakama ya vileo kupinga  maombi  ya wamiliki wa baa lakini mahakama hushindwa  kuyaskiliza  maombi hayo  na kuwapa kipaumbele  wenye mabaa ya kuuza pombe.


Hata hivyo wananchi hao wameiomba Mahakama ya vileo Zanzibar kuacha tabia ya kuwabeba wamiliki wa baa,  kwa kujali fedha wanazotoa  kulipia kibali cha pombe badala yake  kuwatizama wananchi kwa  jicho la huruma kwani baa hizo zimekuwa zikileta athari  katika jamii.

Wamesema  mbali na kuuza pombe lakini pia  hupiga miziki kwa sauti kubwa bila ya kuzingatia  mida ya sala,kuchafua mazingira  katika maeneo ya wananchi  kwa kumwaga ovyo taka zao ikiwemo  chupa na kondom zilizotumika.

Hata hivyo wamesema kuwepo  kwa hali  hiyo imechangia kwa kiasi kikubwa kuporomoka kwa maadili ya vijana na watoto katika jamii kwani inapelekea kuiga matendo wanayoyaona kupitia baa hizo.

Aidha wametoa wito kwa Serikali  ya Mapinduzi Zanzibar kuziondoa baa zote zilizojengwa karibu na makaazi ya wananchi  ili kunusuru vizazi  visiweze kupotea  pamoja na kunusuru afya za  wananchi.

Jumla ya Baa tano leo Pia zilifika Mahakamani kwerekwe kwa ajili ya kufikisha maombi ya kibali cha pombe cha mwaka 2018.

chanzo:

Comments