Wizara
ya Elimu, Sayansi na Teknolojia imepokea taarifa ya kuwepo kwa Taasisi
ya Msaada wa kijamii Tanzania (Tanzania Social Support Foundation -
TSSF) ambayo inajitangaza kuhusika na kutoa mikopo yenye riba nafuu kwa
wanafunzi wa Elimu ya Juu.
Katika
Gazeti la Mwananchi Toleo Namba 6306 la Novemba 2, 2017 katika ukurasa
wake wa Pili iliandika habari iliyosomeka: “Taasisi Yasisitiza Neema
Mikopo Elimu ya Juu.” Habari hiyo pia inaelezea juu ya kuwepo kwa
mkutano Novemba 30, 2017 kati ya TSSF na Wakuu wa Taasisi za Elimu ya
Juu.
Wizara
inapenda kuutangazia Umma kuwa Taarifa hizo siyo za kweli kwani TSSF
haitambuliwi na Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia na tayari Wizara
imeanza kufuatilia kujua uhalali wa usajili wake, hivyo wananchi hawana
sababu ya kuamini kinachotangazwa na Taasisi hiyo.
Wizara
inaziomba Taasisi nyingine za Serikali hasa zinazosajili Taasisi za
Kiraia kufanya uchunguzi wa kina ili kujiridhisha na usajili wake.
Wakati
huohuo, Wizara inamwagiza Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi hiyo ya TSSF, Bw.
Donati Salla, au mwakilishi wake kufika Makao Makuu ya Wizara ya Elimu,
Sayansi na Teknolojia, akiwa na nyaraka zote muhimu za utambulisho wa
Taasisi yake. Akifika aonane na Katibu Mkuu wa Wizara.
Imetolewa na kitengo cha Mawasiliano
WIZARA YA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA.
chanzo:Mpekuziblog.
Comments