Wizara ya Afya Zanzibar imeanza kutoa elimu ya afya katika shehia ambazo kwa kiasi kikubwa zilikubwa na maradhi ya mripuko ikiwemo kipindupindu ili wananchi waanze kuchukua tahadhari mapema hasusan katika kipindi hichi cha mvua za vuli zinazoendelea kunyesha.
Akizungumza na Zanzibar24 Mkurugenzi wa kinga na elimu ya afya Zanzibar Dk.Fadhil Muhamed Abdalla amesema Wizara imejipanga kikamilifu kukabiliana na ugonjwa huo kwa utoaji wa elimu kwa wananchi ili kuhakikisha mvua zinazoendelea kunyesha hazisababishi maradhi.
Amesema kuwa miongoni mwa Shehia ambazo zimepewa kipaumbele katika utowaji wa elimu hiyo ni Mtopepo,Daraja bovu,Kinuni na baadhi ya maeneo ya Vijijini yaliyozungukwa na ukanda wa pwani.
Aidha Dk.Fadhil amefahamisha kuwa mbali na utoaji wa elimu hiyo pia Wizara tayari imeshaweka vifaa vya kutosha katika kila kituo cha Afya ili kukabiliana na maradhi hayo endapo watajitokeza wagonjwa wa maradhi hayo ili kuweza kupatiwa huduma za matibabu kwa haraka.
chanzo:zanzibar24
Comments