Mkurugenzi wa Uchaguzi wa NEC, Ramadhani Kailima alisema hayo jana mchana, ikiwa ni siku moja baada ya Ofisi ya Spika Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutoa taarifa kuwa wameshawasilisha barua kwa mkurugenzi huyo kumtaarifu shauri la Nyalandu la kupoteza sifa za kuwa mbunge.
Kailima alisema, “Mpaka sasa hatujapata taarifa yoyote kuhusu mheshimiwa Nyalandu, kama taarifa hiyo itafika kwetu tutatoa taarifa kwa umma”. Akitoa ufafanuzi kuhusu sheria zinazopaswa kufuata, alisema kuwa Ubunge unaweza kukwama pale mbunge au mbunge wa viti maalumu atakapovuliwa uanachama na chama cha siasa, au kuamua kuachana na chama.
chanzo:Habarileo.
Comments