Ng’ombe hao walikamatwa hivi karibuni katika wilaya hiyo wakitokea Uganda na kukamatwa.
Mpina alisema uvamizi wa kundi kubwa kama hilo la wanyama linaweza kusabisha madhara katika mazingira kama vile mmomonyoko wa ardhi, uharibifu wa vyanzo vya maji, kumaliza malisho ya mifugo iliyoko nchini, kusababisha migogoro ya mara kwa mara kwa wakulima na wafugaji na hata kuleta maambukizi ya magonjwa ya wanyama.
Mpina alisema suala hilo haliingiliani na ushirika wa Afrika Mashariki kwani ushirika huo upo kisheria, hivyo wavamizi wanaoingiza mifugo kinyemela nchini kutoka nchi jirani ni wahalifu kama wahalifu wengine. “Kwa hiyo naangiza ng’ombe hawa 6,648 waliokamatwa hatua ziendelee na ambao hawajakamatwa wakamatwe na wataifishwe na serikali.” alisisitiza. Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Misenyi, Denis Mwila alisema utaratibu wa kutathmini ng’ombe katika wilaya yake bado unaendelea na taratibu za kisheria zinafuatwa.
chanzo:Habarileo.
Comments