
Takriban viongozi 13 wa mataifa tofauti wanatarajiwa kuhudhuria hafla hiyo.
Kiongozi
wa upinzani Raila Odinga ambaye alisusia marudio ya uchaguzi ameitisha
kufanyika kwa mkutano wa upinzani licha ya mkutano huyo kupigwa
marufuku.

Marudio
ya uchaguzi wa Oktoba 26 ulimpatia Uhuru Kenyatta asilimia 98 ya kura
huku waliojitokeza kushiriki katika shughuli hiyo wakiwa asilimia 39.
Sherehe hiyo ya siku ya Jumanne inayofanyika katika uwanja wa
michezo wa Kasarani jijini Nairobi inatarajiwa kuanza mwenzo wa saa nne.

Naibu wa rais William Ruto, pia ataapishwa.
Miongoni mwa
viongozi wa kigeni wanaotarajiwa ni waziri mkuu wa Israeli Benjamin
Netanyahu, rais wa Uganda, Yoweri Museveni na rais wa Rwanda Paul
Kagame.

Maafisa wapolisi wameonya upinzani huo dhidi ya kufanya mkutano huo.
chanzo;Bbc.
Comments