WAVUVI kisiwani Pemba, washauriwa kuitumia na kuifanyia kazi sheria ya Uvuvi namba.7, ya mwaka 2010.

Image result for wavuviWAVUVI kisiwani Pemba, wanashauriwa kuitumia na kuifanyia kazi sheria ya Uvuvi namba.7, ya mwaka 2010, ili kuwa na uvuvi endelevu na wenye tija kwa faida yao na taifa.

Kaimu Afisa Mkuu idara ya maendeleo ya Uvuvi Pemba, Ali Said Hamad, ameyasema hayo katika kambi maalum ya kuwajengea uelewa wavuvi wadogo wadogo huko wesha Wilaya ya Chake Chake.

Afisa huyo amesema kuwa, wavivi wote wanajukumu la kuisoma na kuifuta sheria na sera iliopo kwani ukiukwaji wa sheria hio ndiko kunakochangia uharibifu wa mazingira ya bahari na kupelekea uvuvi haramu.

 
Kwa upande wake, Afisa Uvivi , Hidaya Khamis Hamad, amesema kuwa, sheria haikuekwa kuwakomoa wavuvi bali ipo kutoa maelekezo sahihi yatakayoweza kumpatia mwanajamii mazao yenye kiwango kinachostahiki kiuchumi na kipato zaidi.

Sambamba na hayo Afisa Ufugaji , Ali Hatib, amewasisitiza wavuvi hao kuacha kutumia dhana za uvuvi haramu na kufuata maelekezo yanayotolewa na wataalamu kwa faida yao na vizazi vijavyo.

Kwa upande wake, Ramadhan Haji Ramadhan, amechangia kwa kusema kuwa, Serikali inapaswa kuangali utaratibu wa kuwatafutia vyombo wavuvi wa Zanzibar ambapo zitasaidia kwenda kuvua maji marefu jambo ambalo lisasaidia kutoa ajira kwa
wananchi waliowengi hasa wanaoekeza katika rasilimali za bahari. 

Aidha ameishauri Serikali kupitia taasisi husika kuwaangalia zaidi walioekeza katika shughuli za uvuvi wakati unaporuhusu kuona kuwa wanafaidika katika shughuli zao.

Comments