
Kwamujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini Magharibi Kamishna
msaidizi Muandamizi wa Polisi Hassan Nassir Ali amesema tukio la kwanza
limetokea majira ya saa 3 Usiku
wa kuamkia jana huko amani kwa mabata
baada ya gari isiyofahamika wala dereva kumgonga mwenda kwa miguu alie
tambuliwa kwa jina la Kardudi Mambo mwenye umri wa miaka 35 mkaazi wa
kwamabata na baadae na gari hiyo kukimbia ambapo mpatwa na ajali
alipata maumivu makali mwilini na kulazwa Hospitali ya Mnazi Mmoja na
kufariki majira ya saa 2 asubuhi.
Tukio la pili limetokea jana majira ya saa10 Alfajiri huko Amani
viwanda vidogo vidogo baada ya gari yenye namba za usajili Z872GH aina
ya Noha iliyokuwa ikitokea viwanja vya starehe umaarufu mjini joto
kuacha njia na kupinduka.
Katika ajali hiyo Ameri Haji Makame mwenye umri wa miaka 20 mkaazi wa
melinne Fuoni amefariki duninia na Maryam Madaraka Iddi mwenye umri wa
miaka 25 mkaazi wa melinne amepata jeraha la kichwa na amelazwa
Hospitali ya Mnazi mmoja kwa matibabu.
Hadi sasa Dereva pamoja na wengine waliokuwemo katika gari hiyo hawafahamiki walipo.
chanzo: zanzibar24.
Comments