
Akizungumza na Waandishi wa habari baaada ya mkutano wa kuwasilisha
ripoti ya utafiti wa Maradhi ya kichocho hapa Zanzibar amesema kupungua
kwa maradhi kunatokana na mwamko wa wananchi kutumia dawa za kujikinga
na maradhi hayo.
Amesema katika kuhakikisha maradhi hayo yanaondoka nchini Wizara ya
afya itaendelea na juhudi za kutoa elimu kwa wananchi juu ya kujinga na
maradhi ya kichocho ikiwemo kuacha kutumia maji yaliotuama katika
madibwi ambayo sio salama kwa matumizi ya binaadamu.
Amesema mbali na mafanikio hayo lakini kuna baadhi ya Shehia bado
zinakabiliwa na maradhi hayo ikiwemo Chaani , Kitope na mwera kwa unguja
na Chambani ,Uwandani na kitongoji kwa Pemba.
Aidha amesema katika kubabiliana na maradhi hayo wizara ya afya
inaendeelea na juhudi za kutoa elimu ya kujinga na maradhi ya akichocho
ikiwemo wananchi kutumia Vyoo ,kuacha kutumia maji ya mito badala yake
watumie Maji safi na Salama ili kuepukana na maradhi hayo .
Utafiti huo umefanywa na Mradi wa SCORE ambao umeazishwa mwaka 2002
hapa Zanzibar ukiwa na lengo la kuangalia namna ya kupambana na maradhi
ya kiichocho Nchini.
chanzo: zanzibar24.
Comments