Kiongozi huyo jana aliwataka wafuasi wake kubaki nyumbani na kutoshiriki uchaguzi huo.
Barabara inayoelekea kituo cha Shule ya Msingi ya Olympic ilifungwa na polisi walilazimika kutumia nguvu za ziada kuondoa mawe na matofali yaliyokuwa yamepangwa barabarani.
Katika maeneo ya miji ya Kusumu na Mombasa ambayo ni ngome kuu ya Odinga, kumekuwa na idadi ndogo ya watu wanaojitokeza kupiga kura huku maofisa wa Tume ya Uchaguzi wakiwa wanasubiria wapigakura.
Rais Uhuru Kenyatta amesema hali ya usalama itaimarishwa nchini kote na amewataka Wakenya kwenda kupiga kura, huku wakizingatia haki za wale ambao hawataki kushiriki kupiga kura
Soma: Taharuki yagubika uchaguzi wa marudio nchini Kenya
chanzo:Mwananchi.
Comments