Wazee
wa Kigoma wakiwakilishwa na Mwenyekiti wa Ngome ya Wazee ya Chama cha
ACT Wazalendo, Alhaj Jaffar Kasisiko wamesikitishwa na kauli aliyotoa
Spika Ndugai kuwa anaweza kumzuia Zitto Kabwe asiongee chochote mpaka
ubunge wake utakapokwisha.
Wazee
hao wanasema kitendo cha Spika kumzuia Zitto Kabwe kuongea bungeni ni
sawa na kuwazuia wao wasiongee na shida zao zisiweze kutatuliwa na kudai
inaonekana hiyo kauli imeshafanyiwa kazi na kitendo cha kumwita Zitto
kwenye Kamati ni sawa na kupoteza muda tu na kudai jambo hilo
halimtendei haki kijana wao Zitto Kabwe na wao wenyewe.
Aidha
wazee hao wamemtaka Spika Job Ndugai na viongozi wengine wasiwe na
kiburi na watazame mambo ambayo yanawaunganisha kwa pamoja.
chanzo:Mpekuziblog.
Comments