Wazee wa Mkoa wa Kigoma wakerwa na kauli ya Spika wa Bunge, Job Ndugai.

Wazee wa Kigoma wakiwakilishwa na Mwenyekiti wa Ngome ya Wazee ya Chama cha ACT Wazalendo, Alhaj Jaffar Kasisiko wamesikitishwa na kauli aliyotoa Spika Ndugai kuwa anaweza kumzuia Zitto Kabwe asiongee chochote mpaka ubunge wake utakapokwisha.

Wazee hao wanasema kitendo cha Spika kumzuia Zitto Kabwe kuongea bungeni ni sawa na kuwazuia wao wasiongee na shida zao zisiweze kutatuliwa na kudai inaonekana hiyo kauli imeshafanyiwa kazi na kitendo cha kumwita Zitto kwenye Kamati ni sawa na kupoteza muda tu na kudai jambo hilo halimtendei haki kijana wao Zitto Kabwe na wao wenyewe.

Aidha wazee hao wamemtaka Spika Job Ndugai na viongozi wengine wasiwe na kiburi na watazame mambo ambayo yanawaunganisha kwa pamoja. 
chanzo:Mpekuziblog.

Comments