
Amesema katika siku za hivi karibuni kumekuwa na lawama ya ukosefu ya
uwajibikaji kutoka kwa baadhi ya watendaji jambo linalorejesha nyuma
juhudi za serikali za kuwaletea wananchi huduma za afya bora .
Bakari ameyasema hayo huko hospitali ya Chake chake wakati
akizungumza na kamati ya uongozi ,madaktari na baadhi ya watendaji
kufuatia malalamiko yanayotolewa na baadhi ya wagojwa wanaolazwa
hospitalini hapo
Nao baadhi ya watendaji waliokuwa katika kikao hicho wamekiri kuwepo
kwa mapungufu ya kibinadamu huku wakisema uchache wa wahudumu pia
huchangia kukosekana kwa huduma ya haraka kwa wagonjwa wanapo pokelewa
kwa vile wengine huhitaji huduma ya dharura .
Hata hivyo wameahidi kuyafanyia kazi mapungufu yaliyojitokeza na kwamba hayatatokea tena.
chanzo: zanzibar24
Comments