Wanaharakati wa asasi za kiraia watakamabadiliko.

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar imewasisitiza  wanaharakati wa asasi za kiraia  kufanyakazi  kwa kufuata misingi ya utawala  bora ili kwenda sambamba na  maslahi ya taifa.

Akizungumza katika Tamasha la kumi na moja la asasi za kiraia Zanzibar Naibu katibu Mkuu Wizara ya katiba,Sheria,Utumishi wa Umma na Utawala bora Mashaka Kubingwa Simba amesema uwepo wa asasi za kiraia  nchini unasaidia katika utekelezaji wa majukumu  mbalimbali ya serikali   hivyo ni vyema  kuwa makini katika  utekelezaji huo kwa kufuata  misingi ya utawala bora.


Naibu katibu Mkuu Wizara ya katiba,Sheria,Utumishi wa Umma na Utawala bora Mashaka Kubingwa Simba.
Aidha amesema  katika  kutekeleza  misingi ya utawala bora katika jamii serikali  imeweka mipango madhubuti  katika  kupambana na suala la rushwa na uhujumu uchumi ili kuziba mianya ya upotevu wa mali za umma kwa lengo la kudumisha misingi ya utawala bora.

Akizungumzia suala la ugatuzi  amewataka wanaasasi hizo  kuwashajihisha  wananchi  masuala ya ugatuzi kwani  serikali imo katika  mchakato wa kuyatekeleza kupitia  baadhi ya sekta zake ikiwemo elimu,afya na kilimo.

Nae Mwenyekiti wa Mwavuli wa asasi za kiraia Zanzibar Asha Aboud Mzee amesema asasi zimeweza kupata mafanikio  makubwa tangu kuazishwa kwa matamasha yake  ikiwemo  ni pamoja na  ushirikishwaji  mkubwa katika  mipango  ya uchambuzi  wa sera na sheria  katika  baadhi ya sekta za serikali.

Hata hivyo  amesema  kuwa  ni vyema  serikali  kutoa nguvu zaidi  kwa asasi  hizo ili  kuweza kuleta  mafanikio na maendeleo  kwa wananchi  kama ilivyodhana  ya utawala  bora nchini

Mwenyekiti huyo  pia ametoa wito  kwa watendaji wa asasi za kiraia nchini kutovunjika moyo  katika kupigania haki za wananchi  katika kuleta  dhana  ya utawala bora na watumie  misingi  ya usawa na haki katika kufanikisha hilo.

Kwaupande wake Mkurugenzi  wa mfuko wa kusaidia asasi za kiraia kutoka  Dar es salamu Profesa Honest Ngowi amesema katika kuhakikisha asasi  hizo  zinapanda  chati  katika kuleta maendeleo  wamekuwa wakizipatia nguvu azaki  zote  ili ziweze kutoa  misaada zaidi katika jamii kwa kukuza maendeleo  na uchumi wa nchi.

Mapema wakichangia mada  ya utawala bora nchini baadhi ya wadau walioshiriki katika tamasha hilo akiwemo  Abdul-wahid Sariboko kutoka Suza,Khadija Abdul-haji kutoka Zanzibar youth forum wamesema nivyema  asasi za kiraia  kuwa mstari wa mbele  katika kutoa  ushauri juu ya mipango mbalimbali ya serikali  kwalengo la kuleta ufanisi wa utawala bora.

Hata hivyo wamesema  asasi zihakikishe  zinashiriki katika  upangazi wa mipango ya utekelezaji  na upimaji wa tathimini ya utekelezaji wa mipango  hiyo  hasa katika  mipango ya elimu,afya bora, chakula,malazi,ajira,uhuru na kuzingatia  haki na usawa  katika utendaji wao wa kila siku.

Aidha  wamesema katika kutekeleza azma ya utawala bora lazima mambo muhimu yafanyiwe kazi  kama vile rushwa,udhalilishaji,migogoro ya ardhi,mfuko wa haki jinai  kuwa rafiki  kwa jamii ya watu wenye ulemavu pamoja na kutafutiwa ufumbuzi wa ucheleweshwaji wa kesi mahakamani.

Tamasha hilo la kumi na moja la asasi za kiraia litafanyika  siku mbili ambapo litajadili mambo mbalimbali ya utawala bora ambapo kauli mbiu yake ni misingi ya utawala bora na ustawi wa asasi za kiraia Zanzibar.

chanzo:zanzibar24.

Comments