Wabunge wa upinzani waendeleza mgomo Bungeni.

leo Septemba 12, 2017 wabunge waupinzani wamegoma kwa mara nyengine na kutoka nje ya bunge wakigomea kuapishwa kwa wabunge wateule wa Chama cha Wananchi CUF.

Septemba, 5 mwaka huu pia wabunge hao walionekana wakigoma na kutoka nje ya bunge  wakieleza kutounga mkono kitendo cha kuapishwa kwa wabunge Saba wa CUF ya lipumba pia wamefanya hivyohivyo na leo ambapo alikuwa akiapishwa mbunge mmoja aliyebakia kati ya wale saba walioapishwa.


Mbunge wa Viti Maalum CHADEMA Suzan Lyimo amesema wameamua kutoka nje baada ya kuona ‘Order Paper’ ikionesha kuna Mbunge wa CUF anaapishwa na kusema wataendelea kususia tukio lolote linalohusisha wabunge hao wapya wa CUF.

Kumekuwepo na mgogoro ndani ya CUF hali iliyopelekea kuwepo kwa makundi mawili moja likiwa ni kundi linalomuunga mkono Mwenyekiti wa CUF anayetambuliwa na Msajili wa vyama vya siasa Profesa Lipumba, huku kundi lingine likiwa ni upande wa Katibu Mkuu wa CUF taifa Maalim Seif.
chanzo: zanzibar24.

Comments