
Akitowa taarifa kwa Waandishi wa Habari Naibu Mkurugenzi wa Idara
ya Habari Maelezo Zanzibar Dk.Juma Muhammed Salum amesema serikali
ilichukuwa hatua mbali mbali ikiwemo kusambaza mafuta ya hakiba hadi
meli hiyo ilipowasili September 14 ili kupunguza tatizo hilo kwa
wamiliki wa Vyombo vya moto.
Hata hivyo amesema serikali kupitia mamlaka ya udhibiti wa huduma za
maji na nishati ZURA imebadilisha mfumo wa uletaji Mafuta hapa Zanzibar
kuazia septemba mosi mwaka huu kutoka katika makampuni manne ambapo kwa
sasa itakuwa ni kampuni moja itakayoshinda zabuni.
Amesema kwa chini ya utaratibu huo utawezesha mafuta kuletwa moja
kwa moja Zanzibar baada ya utaratibu wa awali wa mafuta kuchukuliwa
kutoka dare s salaam na Mombasa.
Aidha amesema mpaka sasa kampuni inayohusika kuleta mafuta ni kampuni ya AUGUSTA ENERGY kutoka Switzerland.
Kutokana na utaratibu huo mpya serikali imesema itakuwa na utaratibu
wa kutangaza zabuni kila baada ya miezi miwili na kuruhusu kampuni
itayoshinda zabuni hiyo kuendeleza uletaji mafuta hapa Zanzibar.
Hivi karibu wamiliki wa Vyombo vya moto walikabiliwa na Tatizo la
ukosefu wa Mafuta katika vituo vya kununulia Mafuta na kupelekea
msongamano mkubwa wa Vyombo vya Moto katika vituo vya mchanzo:Zanzibar24.
Comments