Rais shein afanya uteuzi mwengine katika taasisi mbalimbaili za serikali.

uteuziRais wa Zanzibar Dk. Ali Mohamed Shein amefanya uteuzi wa viongozi katika taasisi mbalimbali za serikali.
Kwa mujibu wa taarifa ya ikulu, rais dk shein amemteua Amour Hamad Saleh kuwa ofisa mdhamini  ofisi ya rais na mwenyekiti wa baraza la mapinduzi-pemba.

Bibi Sabra Issa Machano ameteuliwa kuwa mkurugenzi mwendeshaji wa mfuko wa hifadhi ya jamii Zanzibar (ZSSF), Bibi Salama Ramadhan makame ameteuliwa kuwa kamishna  wa idara ya watendakazi katika tume ya mipango zanzibar.


Aidha Seif Shaaban Seif ameteuliwa kuwa kamishna  wa idara ya mitaji ya umma,  Othman Juma Othman anakuwa mkurugenzi mtendaji wa mamkala ya ununuzi na uondoaji wa  mali za serikali.

Wengine ni Rashid Mohamed Kassim aliyeteuliwa kuwa mkaguzi wa ndani mkuu wa hesabu za serikali, khamis shibu mwalimu mkurugenzi  wa idara ya sera za kodi na fedha katika wizara ya fedha na mipango.

Mohammed Jaffar Jumanne ameteuliwa kuwa mkurugenzi wa idara ya uendeshaji na utumishi katika wizara ya biashara, viwanda na masoko, khamis ahmada shauri, mkurugenzi  wa idara ya biashara na masoko.

Wengine ni dkt vuai iddi lila ameteuliwa kuwa katibu mtendaji wa kamisheni ya utalii, zahor kassim mohamed anakuwa  mkurugenzi  mwendeshaji wa kampuni ya uvuvi ya zanzibar (zafico).

Asha hamid rajab ameteuliwa kuwa mthamini mkuu katika wizara ya ardhi, maji, nishati na mazingira na  ali suleiman ameir anakuwa mkurugenzi wa idara ya ajira katka wizara ya kazi, uwezeshaji, wazee, vijana, wanawake na watoto.

Uteuzi huo unaanza jumatatu septemba 25, 2017
Imetolewa na habari maelezo zanzibar
23 septemba 2017.
chanzo: zanzibar24.

Comments