
Dk. Shein amesema hayo alipokuwa akiongoza kikao cha Kamati Maalum
ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa Zanzibar ambapo amewataka viongozi
kutambua umuhimu wao kushuka chini kwa wananchi na kushirikiana nao
katika harakati za maendeleo na kubaini changamoto zao ili kuzipatia
ufumbuzi na kujenga imani kwa wananchi.
Amesema kuwa viongozi wa Chama na Serikali wana wajibu mkubwa wa
kutimiza wajibu wao kikamilifu katika kukiwezesha Chama na Serikali
kuendelea kukubalika zaidi kwa wananchi na kushinda kwa kiwango cha juu
zaidi katika uchaguzi mkuu ujao 2020.
Mbali na hilo kikao hicho kilipokea na kujadili majina ya wagombea
50 waliojitokeza kuomba nafasi za Uenyeviti wa CCM katika Wilaya 12 za
Unguja na Pemba na kutoa mapendekezo yake ili kuyapeleka katika vikao
husika.
chanzo: zanzibar24.
Comments