
“Sisi tunatoa taarifa za maendeleo ya Lissu kulingana
na Madaktari wanavyotuambia, hatuwezi kusema chochote nje ya wataalam
hao, kwa kuwa ndio wenye ujuzi wa kumtibu na kujua maendeleo ya mgonjwa
husika, Unajua ahueni humtokea mgonjwa taratibu taratibu na ndivyo
inavyotokea kwa Lissu, ingawa sisi wote tuna hamu apone mara moja aje
aendelee kupigania haki za wanyonge kama alivyokuwa akifanya” alisema Mbowe.
Aidha kiongozi huyo amezidi kuwaomba Watanzania kuzidi kumuombea
Tundu Lissu na kuendelea kuchangia gharama za matibabu kwa kiongozi huyo
kwani gharama za matibabu yake ni kubwa mno na wao kama chama peke yao
hawatoweza.
“Kupona kwa Mhe. Lissu ni mpango wa Mungu, nawaomba
Watanzania wenzetu waendelee kumuombea kwa Mungu pamoja na kuchangia
gharama za matibabu, kwa kuwa gharama zake ni kubwa ambazo chama pekee
hakiwezi kuzimudu bila ya misaada kutoka kwa watu mbalimbali” alisisitiza Freeman Mbowe.
Mbunge Tundu Lissu yupo mjini Nairobi Kenya kwenye matibabu
kufuatia kupigwa risasi na watu wasiojulikana Septemba 7, 2017 akiwa
mjini Dodoma na baadaye kusafirishwa na kwenda Kenya kwa matibabu.
chanzo: zanzibar24.
Comments