
Hayo aliyasema katika sherehe za uzinduzi wa shehia mpya ya
Kwamtumwajeni, Baraza la vijana la shehia na kumtambulisha rasmin Sheha
wa shehia hiyo Rajab Ngauchwa zilizofanyika katika Jimbo la Magomeni.
Alisema Vijana wengi wamekuwa wakijihusisha na vitendo viovu katika
jamii jambo ambalo linarudisha nyuma maendeleo yao sambamba na
kujijengea mfumo mbaya wa maisha yao.
Aidha aliwaomaba vijana waliojiunga na baraza la shehiya ya
Kwamtumwajeni kuchukuwa juhudi ya kuwaelimisha vijana wenzao ndani ya
shehia yao na shehia nyengine kujiunga na mabaraza ya vijana.
Aliwaeleza vijana kuwa wanayofursa kubwa ya kujiunga katika mabaraza
hayo kwani hakuna ubaguzi kitu muhimu ni kufuata sheria na taratibu
zilizowekwa.
Mkuu wa Wilaya aliwahakikishia vijana hao kuwa Ofisi yake ipo tayari
kushirikiana nao katika kutafuta maendeleo kwa kuanzisha miradi mbali
mbali itayoweza kuwasaidia katika kujikwamuwa na maisha.
“Wilaya yangu ipo pamoja na nyinyi hivyo ninawasihi vijana msikubali
kuingizwa katika vitendo viovu vitavyosababisha kuharibikiwa katika
maisha yenu na kupoteza muelekeo mzima wa maisha,”alisema Marina.
Muwakilishi wa Jimbo la Magomeni Rashid Makame Shamsi aliahidi kuwa
yupo tayari kushirikiana pamoja na vijana nakuweza kuzitatuwa
chanagamoto zinazowakabili katika shughuli zao.
Aliwataka vijana wa Jimbo la Magomeni kuweza kuzitumia fursa
zinazotolewa na viongozi wao za kujifunza ujasiria mali kwani wataweza
kujisaidia katika maisha yao na kupunguza idadi ya vijana wasio na
ajira.
Muwakilishi Shamsi alisema Vijana wengi wamekuwa wakijihusisha na
vitendo vibaya katika jamii jambo linalorudisha nyuma usalama wao huku
ukizingatia kuwa vijana wa leo ndio nguvu kazi ya taifa lijalo katika
Nchi yetu.
Sambamba na hayo aliwaomba vijana kushirikiana pamoja ili kuweza
kufanya kazi za maendeleo katika jimbo la magomeni na kujikwamuwa katika
mfumo mbaya wa maisha ambao unaowakabili vijana.
Katika sherehe hiyo Muwakilishi Shamsi alimkabidhi vitendea kazi vya
Ofisi Sheha wa shehia ya Kwamtumwajeni na kumuahidi kushirikiana nae ili
kuhakikisha anatekeleza majukumu yake kwa ufanisi.
Akitowa shukurani, Sheha Rajab Ngauchwa alisema yupo tayari
kushirikiana na Wananchi wote wa shehia yake bila ya kubaguwa ili kuweza
kuharakisha maendeleo kwa pamoja.
Aliwataka Wananchi kufuata sheria zilizowekwa katika nchi ili kuepuka
matatizo madogo madogo yanayoweza kujitokeza na kuwasihi kuendeleza
hali ya usalama na amani katika jimbo hilo na jamii kwa jumla.
Alisema kuna umuhimu mkubwa wa kulinda na kuhifadhi mazingira
yanayowazunguka kwa kufanya usafi ili kujiepusha kutokea maradhi mbali
mbali ya mripuko.
Akisoma risala ya shehia hiyo, Mjumbe wa Baraza la Vijana Khadija
Mgasho Mussa alisema katika shehia yao wamefanikiwa kuunda kikundi cha
utunzaji wa mazingira, kuondoa vigenge vya vijana wanaohatarisha usalama
wa wananchi na mali zao pamoja na kudhibiti uingiaji wa wageni
kiholela.
Alimueleza Mkuu wa Wilaya kuwa shehia hiyo inakabiliwa na changamoto
mbali mbali zikiwemo kukosa sehemu ya kuwekea taka, vifaa vya kufanyia
usafi wa mazingira, pamoja na kukosa ofisi kwa ajili ya Baraza la
vijana na vitendea kazi.
chanzo: zanzibar24.
Comments