Jitihada za SMZ zawafurahisha wananchi wa Kikwajuni.

Wananchi wa Jimbo la Kikwajuni wamesema wamefurahishwa na hatua za viongozi wao wa jimbo hilo kwa kulipa umuhimu suala la matibabu ambapo limeweza kuwapunguzia usumbufu wa kufata huduma za afya nje ya Zanzibar.

Miongozni mwa Magonjwa yanayotibiwa  ni mifupa,Presha,Sukar,Uti wa mgongo ambapo matibabu yake yatakuwa bure pamoja na  upatikanaji wa dawa bila ya malipo.

Wakizungumza mara baada ya kupatiwa huduma za afya katika eneo la Rahaleo baadhi ya wananchi hao  Amina Abrahmani,Juma Ali Kitwana wamesema  ujio wa madaktari bingwa katika jimbo lao umeweza kuleta faraja na kusaidia wananchi  kuweza kupata  huduma za afya bure.
Hata hivyo wamewaomba viongozi wao  zoezi hilo la matibabu kuwa endelevu  kwani bado wananchi  wanapata usumbufu sana katika  kumudu gharama za matibabu  hasa ya mifupa.
Nao Viogozi wa Jimbo hilo Mbuge Hamad Yussuf Masauni,Mwakilishi pamoja na Diwani wamesema  ujio wa madaktari bingwa katika jimbo lao ni miongoni mwa ahadi zao walizoziahidi  kwa wananchi wakati wakiinadi ilani ya chama cha mapinduzi.
Aidha wamewaahidi kuzitekeleza  ahadi zote walizoziahidi kwa wananchi awamu kwa awamu ili kuwaondolea  usumbufu  wa huduma mbalimbali zinazowakabili.

chanzo;zanzibar24

Comments