Jeshi la Polisi lawatia mbaroni wanaojiuza Kizimkazi Unguja.

Jeshi la polisi lawabana koo na wamesema hawatowavumilia kamwe.

Walioshindwa kufahamumthamani ya uganajike kwa kujiuza miili yao kwa bei ya seli nyakati za usiku, huko Kizimkazi Mkoa wa Kusini Unguja.

Kina dada hao kutoka mitaa mbali mbali ya mjini ikiwemo kwahani na miembeni kitendo hicho kisichokuwa cha uungwana chawafanya jeshi la polisi Mkoa wa kusini  unguja kuacha vitanda vyao kwa muda kuwavamia kizimkazi mithili ya sega la nyuki na kuwa kamata wakina dada ishirini  pamoja na wateja wao wanaotuhumiwa kufanya vitendo hivyo.


Kamanda wa polisi mkoa wa kusini Unguja Kamishna msaidizi wa Polisi Juma Sadi Khamisi amesema kinadada hao wamekamatwa majira ya saambili usiku wakiwa wapo kwenye mauzo na wateja wao.

Amesema Kuna biashara halali za kujipatia riski kwahivyo si vyema mtu akatumia mwili wake akafanya biashara hizo ambazo ni hatari kwa afya yao na hatari kwa afya za wengine”

Hata hivyo Kamanda Sadi amesema kitendo hicho hakitavumilika Jeshi litapambana vikali ili kieleweke.

chanzo:zanzibar24.

Comments