askari polisi huyo anayetokea katika jimbo la Nakuru nchini Kenya
ambaye alikuwa skari polisi wa kituo cha Molo, amempiga risasi mke wake
mara tatu kwa kutumia bunduki ya AK47 wakiwa nyumbani kwao.
Shuhuda wa tukio hilo ambaye ni mlinzi wa eneo hilo amesema
walisikia kelele za watu wakilumbana, na walipokuwa wakikimbilia kujua
kulikoni walisikia milio ya risasi na kisha kukawa na ukimya.
Majirani wa eneo hilo wamesema walisikia kelele za mtoto akilia kwa sauti huku akisema baba anamuuwa mama.
OCPD wa Nakuru Joshua Omukatta amesema wanaendelea na uchunguzi wa
tukio hilo, huku miili ya marehemu wote ikiwa imepelekwa katika
hospitali ya serikali ya Nakuru.
chanzo: zanzibar24.
Comments