20 mbaroni kwa kujihusisha na mapenzi ya jinsia moja Zanzibar.

alawitiJeshi la polisi mkoa wa mjini magharibi linawashikilia watu 20 kwa tuhuma za kujihusisha na mapenzi ya jinsia moja.

Akizungumza na waandishi wa habari kufuatia tukio hilo huko katika kituo cha polisi madema Kamanda wa polisi Mkoa wa Mjini magharibi Kamishna msaidizi mwandamizi wa polisi Hassan Nassir Ali amesema  watu hao wanawake 12 na wanaume 8 wenye umri kuanzia miaka 18.


Kamanda Nassir amesema vijana waliokamatwa walikuwa katika ukumbi wa hoteli ya Mazson wakiwa katika mafunzo ya kuhamasishana katika vitendo hivyo. Amefahamisha kuwa jeshi la polisi linaendelea na upelelezi wa tukio hilo na limesema halitofumbia macho vitendo hivyo ambavyo vinakwenda kinyume na maadili ya nchi.

Kamanda Nassir amewataka wazazi na walezi kufatilia nyendo za watoto wao kutojiingiza katika vitendo hivyo ili kuokoa vizazi ambavyo ndio tegemezi kwa nchi.

Watu hao wamekamatwa katika mafunzo ambayo yameandaliwa na taasisi ya Bridge Initiative Organization ambayo imesajiliwa Zanzibar kwa lengo la kutoa elimu ya ukimwi lakini badala yake inahamasisha mapenzi ya jinsia moja.
chanzo: zanzibar24.

Comments