
![]() |

Akizungumza wakati alipotembelea jengo la mahakama hiyo amesema
kusuasua kwa ujenzi huo kunapelekea kukwamisha harakati mbalimbali za
watendaji wa mahakama hiyo jambo ambalo linalorudisha nyuma shughuli
nyingi za maendeleo.
Waziri Haroun amesema ameridhishwa na hatua zilizofikiwa katika
ujenzi wa mahakama hiyo kujengwa vyumba vya kutosha, utanuzi wa kumbi
za mahakama kwa ajili ya kuskilizia kesi pamoja na ofisi za mahakimu.
![]() |
Kwaupande wake Naibu Mrajisi Mahakama kuu Zanzibar Khamis Ramadhani
Abdalla amesema kutokana na uchakavu wa jengo hilo lilivokuwa awali
serikali kwa makusudi imeamua kulijenga upya ili kunusuru maisha
ya wananchi kwani lilikuwa katika hali mbaya.
Amesema jengo hilo lina umuhimu mkubwa kumalizika
kwake kwani kesi zote zinazotokea katika wilaya ya mjini na magharibi
za wananchi zinapelekwa katika mahakama hiyo ya wilaya
mwanakwerekwe.
Aidha amesema pia jengo hilo likiwa katika
mazingira mazuri litaweza kusaidia mahakimu kufanya kazi katika
mazingira bora hasa katika utendaji wa kazi zao.
Zaidi ya Shillingi Milioni Mia moja na thalasini na tano zimetumika katika ujenzi huo wa mahakama.
Chanzo: zanzibar24.
Comments