
DPP alikuwa amefungua maombi Mahakama ya Rufani akiomba kibali cha
kufungua maombi ya mapitio kutokana na uamuzi wa Mahakama Kuu kumfutia
Lwakatare mashtaka ya ugaidi.
Maombi ya DPP yalitarajiwa kusikilizwa leo Ijumaa, Agosti 11 na
Jaji wa Mahakama ya Rufani, Mussa Kipenka, lakini wakili wa serikali
Mkuu, Tumaini Kweka ameiambia mahakama kuwa DPP hana nia ya kuendelea na
maombi hayo kutokana na uamuzi wake wa kuyaondoa maombi hayo kabla ya
usikilizwaji.
Kutokana na hatua hiyo wakili wa mjibu maombi, Richard Rweyongeza
amesema hana pingamizi dhidi ya maamuzi hayo ya DPP pia na Jaji Kipenka
akatoa amri ya kuyaondoa mahakamani maombi hayo.
Hivyo kwa sasa Lwakatare anabaki na shtaka la kula njama ili
kutenda kosa, katika kesi ya msingi inayosikilizwa na Mahakama ya Hakimu
Mkazi Kisutu.
Lwakatare na mwenzake Ludovick Rwezaura walikuwa wanakabiliwa na
jumla ya mashtaka manne yakiwemo ya kufanya ugaidi na kula njama za
kufanya vitendo vya kigaidi kwa lengo la kumdhuru kwa sumu aliyekuwa
Mhariri wa gazeti la Mwananchi, Denis Msacky.
chanzo: zanzibar24.
Comments