
Kamanda msaidizi, muandamizi wa jeshi la polisi wa mkoa wa mjini
magharibi, Hassan Nassir Ali amemtaja kijana huyo, Omar Ali Hajji (29)
mkaazi wa Bububu,
kuwa tarehe 31 julai 2017 asubuhi alitaka kujipatia
fedha kwa njia ya udanganyifu kutoka kwa mgonjwa aliyefika kupata huduma
hospitalini hapo na badala yake kufanya uhalifu wa kumtorosha mtoto.
Kamanda Nassir amefahamisha kuwa mtuhumiwa huyo alidai shilingi elfu
kumi kutoka kwa mama wa mgonjwa ili awapatie dawa za matibabu lakini
baadae aligundulika kufanya hila ndipo alipokamatwa na kufikishwa
polisi.
Akielezea tukio hilo, Mama wa mtoto huyo Mariam Suleiman Hamad
amesema baada ya kumpa pesa daktari feki huyo, alimtilia shaka na kuamua
kumfuatilia ndipo alipobaini kutaka kutoroka huku akiwa tayari
amemchukua mtoto wake.
Aidha Kamanda nassir ametoa wito kwa wazazi wanaofika hospitalini
hapo kuwa makini na watoto wao wanaofika nao kwenye hospitali ili
kuepuka vitendo vinavyoweza kujitokeza kwa baadhi ya watu amabao hawana
imani nzuri na pia kumpongeza mama huyo kwakuwa na hamasa ya kulikabili.
chanzo: zanzibar24.
Comments