
Kamanda wa Polisi, Mkoa wa Arusha, Charles Mkumbo, alisema tukio
hilo lilitokea juzi katika Kijiji cha Engalaoni kilichopo mpakani mwa
wilaya za Monduli na Arumeru.
Kamanda Mkumbo amesema Rubani huyo, alikuwa akiendesha ndege ndogo
yenye namba za usajili 5HSAL 206 inayomilikiwa na Kampuni ya Safari Air
Link.
“Ndege hiyo yenye uwezo wa kubeba abiria watano,
iliondoka katika uwanja mdogo wa ndege wa Arusha, majira ya saa 1:30
asubuhi siku hiyo ya tukio ikielekea katika eneo la Kogatende, Serengeti
kuwachukua watalii.
“Kwenye ndege hiyo, alikuwamo rubani peke yake na alikuwa anasubiriwa na watalii huko Serengeti.
“Taarifa za kuanguka kwa ndege hiyo zilianza kuenea
juzi saa nne asubuhi, zikisema kuna ndege imeanguka katika vilima vya
Monduli ambavyo ni maarufu kama Monduli Hills.
“Baada ya taarifa hizo kutolewa saa 6:30, tuliwajulisha
kikosi cha zimamoto na wenzetu wa uwanja wa ndege wa Arusha na
walipofika kwenye kilima hicho, walikuta rubani ameshafariki dunia na
mwili wake ulichukuliwa kwa uchunguzi zaidi,” alisema Kamanda Mkumbo.
Hivyo Kamanda Mkumbo amesema uchunguzi wa tukio hilo umeanza na
watashirikisha na wataalamu waliobobea katika masuala ya ndege ili
uchunguzi huo uende kiufasaha zaidi.
Chanzo: zanzibar24.
Comments