
Hii inatokana na kuwepo kwa mfumo wa utoaji wa risiti kwa mkono ambao
unaonekana kuwa na matatizo mengi na kupelekea kukosesha Serikali
mapato yake.
Akitoa mafunzo kwa waandishi wa habari huko katika kiwanja cha
Gombani Chake Chake juu ya matumizi ya Mashine hizo Mkuu wa idara ya
sera utafiti na mipango ZRB Nd. Khamis Saadati amesema, utoaji wa risiti
kwa kutumia mashine za kielectroniki ni mfumo wa kisasa ambao unatumika
katika kutunza kumbukumbu na kuondoa udanganyifu katika ulipaji kodi
kwa wafanya biashara.
Amefahamisha kuwa mfumo huo utamuwezesha mteja kupatiwa risiti halali
yenye kuonesha uhalali wa bidhaa aliyo nunua pamoja na bei
aliyonunulia.
Kwa upande wake Mkuu wa Idara ya Teknolojia ya mawasiliano (ICT)
ndugu Mussa Amour Ali amesema, wafanya biashara wanauwezo wa kuichezea
mifumo ya zamani ya utoaji risiti na kupelekea kukosekana kwa mapato
lakini kwa mfumo huu wa kisasa hautowez a kufanya hivyo kwani mashine
hizo zitakuwa zikiendeshwa na ZRB wenyewe.
Amefahamisha kuwa endapo mfanya biashara hatopeleka taarifa za mauzo kwa ZRB basi bodi hiyo itapata ripoti kupitia mashine hiyo.
Mkuu huyo amesema Mashine hizo hawatafungiwa wafanya biashara tu bali
maeneo yote hadi kwenye taasisi za Serikali ili kuzuia mwanya wa
ukwepaji kodi.
chanzo: zanzibar24.
Comments