
Kauli hiyo imetolewa jana na katibu wa wazazi wilaya ya chakechake
Bikiembe Ramadhan Khamis katika zoezi la ugawaji fomu za kugombea nafasi
mbalimbali katika jumuia hiyo, zoezi ambalo limeanza rasmin tarehe 2
jully 2017.
Akimkabidhi fomu ya ugombea nafasi ya wajumbe wawili wa halmashauri
kuu wilaya ya chakechake mmoja miongoni mwa wagombea hao Bimkubwa Rajab ,
Bikiembe amefahamisha wagombea hao kuwa, katika kinyang’anyiro hicho
kuna kupata na kukosa, hivyo kwa wale wote watakaokosa nafasi
wanazozigombania wasiwe wenye kuvunjika moyo na badala yake waendelee na
utumishi mzuri katika chama kwani haiwezekani kupata wote
waliyojitokeza kuomba.
Akipokea fomu hiyo Bimkubwa Rajab ametoa wito kwa wanachama wenzake
kumunga mkono ili kuhakikisha anapata nafasi hiyo huku akiahidi kuingia
vijijini kuwatafuta akina mama kuwashajihisha kujiunga na chama sambamba
na kuwasemea changamoto zao zinazowakabili.
Kwa pande wake Seif kassim mwanamacha wa chama hicho anaegombea
uwenyekiti wa wazazi wilaya ya chakechake amesema, ni vyema kwa
wanachama hicho kuutumiwa wakati huu kugombea nafasi mbalimbali za
uwongozi kwani kutaleta maendeleo makubwa katika chama.
Amesema ikiwa kuna mwanachama anaona kuna kiongozi
hatekelezi majukumu ipasavyo basi huu ndio wakati muwafaka kuchukua
fomu na kugombea ili kurekebisha pale ambapo aliona hapakua sawa.
Kila baada ya miaka mitano chama cha mapinduzi CCM na jumuiya zake
hufanya chaguzi za viongozi mbalimbali ikiwa ni katika muendelezo wa
matumizi ya democrasia katika chama hicho.
chanzo: zanzibar24.
Comments