
Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa Diwani wa kata hiyo Innocent
Kukongwa alisema watu hao walikula ugali wa muhogo ambao ulikuwa
umeandaliwa kama chakula cha usiku ,ambapo baada ya
kulawalianzakuharisha na kusababisha watoto wawili kufariki dunia na
wengine sita kukimbizwa zahanati kwa matibabu zaidi.
Amefahamisha kuwa baada ya kutumia chakula hicho waliamua kutumia
dawa ya kienyeji badala ya kwenda hospitali na kusababisha kifo kwa
watoto hao.”Inasikitisha kwani baada ya kula chakula hicho hawakutaka
kwenda zahanati na badala yake waliendelea kujitibu kwa kutumia miti
shamba na kushtuka baada ya kuona hali bado ilikuwa ikiendelea kuwa
mbaya”,alisema Kukongwa.
Kwa upande wake Afisa tarafa ya Kasanga Peter Mankambila
amesema kwa kawaida ugali wa muhogo huliwa maara baada ya kurowekwa kwa
zaidi ya siku tatu inaonyesha familia hiyo ilikula ugali huo bila ya
kuroweka vizuri.
“Muhogo unaolimwa kwenye maeneo haya ya Mwambao wa Ziwa
Tanganyikahuwa ni mchungu kupita kiasi, hivyo bila kuuloweka vizuri ni
lazima ukuletee madhara kiafya kama ilivyotokea kwa familia
hii”,alieleza.
Nae Kamanda wa polisi mkoa wa Rukwa Geoge Simba Kyando alisema kuna
taarifa mchanganyiko juu ya tukio hilo na kuahidi kutoa taarifa zaidi
mara baada ya uchunguzi.
“Kuna taarifa tofauti kwenye tukio hili, kwani inadaiwa kuwa
familia hiyo ilitumia dawa ya kienyeji na zingine zinadai kuwa walitumia
ugali wa muhogo hivyo tunashindwa kupata taarifa sahihi ni zipi,
tutatoa taarifa zaidi uchunguzi ukikamilika na kubaini chanzo halisi cha
vifo vya watu hao’’,alisema kamanda Kyando.
chanzo: zanzibar24.
Comments