Wananchi wametakiwa kuchangamkia fursa zilizopo katika kampuni ya Fumba Town development ambazo zitakazoweza kuwapatia ajira na kupata huduma nyengine za kijamii.
Akizungumza na Waandishi wa habari huko ofisini kwake mazizini Afisa Mtendaji wa kampuni hiyo Tobias Dietzold amesema tokea kuanzishwa mradi wa Fumba wa kujenga nyumba pamoja na mambo mengine ya maendeleo muitiko kwa wananchi umekuwa mdogo kujitokeza kuomba nafasi za ajira na kuwahimiza wananchi kujitokeza ili kuweza kushiriki katika shughuli mbalimbali za kimaendeleo.
Hata hivyo amesema mradi huo utaweza kuwanufaisha wananchi katika Nyanja za maendeleo lengo ni kuboresha maisha ya watu kimakaazi pamoja na kuweka huduma za kijamii katika maeneo ya nyumba hizo ambazo zitawanufaisha wananchi walio wengi ikiwemo skuli,hospitali ya kisasa pamoja na huduma ya maji safi na salama.
Amesema tokea kuanzishwa mradio huo oktoba mwaka 2015 hadi mwaka huu2017 nyumba takribani 80 za ghorofa zimekamilika na malengo ya mradi huo ni kujenga nyumba Elfu 1020.
chanzo:Zanzibar24
Comments