Tanzania yaombwa kuisaidia sudan kusin kwa sekta tofauti.

Sudan Kusini imeoimba Tanzania kuisaidia kutoa mafunzo  kwa wataalamu wake husasani katika sekta ya afya, kilimo na kupatiwa walimu wa lugha la Kiswahili.

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Sudan Kusini Jenerali Taban Deng Gai ameeleza taifa lao linataka  kufundisha lugha ya kiswahili katika shule mbalimbali nchini humo.

maombi hayo ameyatoa wakati alipo kutana na kufanya mazungumzo na Makamu wa Rais wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kando ya Mkutano wa  29 wa Wakuu wa Nchi na Serikali ya Umoja wa Afrika Jijini Addis Ababa Ethiopia.


Pia Jenerali Taban Deng ametoa shukurani kwa Serikali ya Tanzania kwa kuiunga mkono  Serikali ya Sudan Kusini kupitia Jumuiya mbalimbali hususan Jumuiya ya Afrika Mashariki katika harakati zake za kupambania amani ya kudumu sambamba na kuwavumilia kipindi chote wanapopitia changamoto kufikia amani hiyo.

Kiongozi huyo amesema  taifa lao bado ni changa barani Afrika hivyo ipo haja  Serikali ya Tanzania kulisaidia  ili liweze kuimarisha kiulinzi na usalama pamoja na uimarishaji wa utoaji wa huduma za msingi kwa wananchi wake.

Nae makamo wa rais wa Tanzania Samia  Suluhu Hassan amesema ili Tanzania iweze kushirikiana vizuri na Serikali ya Sudan Kusini ni lazima Wizara ya Mambo ya Nje na Ushikiriano wa Kimataifa za nchi hizo Mbili kuandaa mfumo maalum wa ushirikiano na utekelezaji wake.

Mfumo utakao ainisha maeneo ya kushirikiana katika sekta tofauti ikiwa katika  sekta za afya, elimu, kilimo, siasa, ulinzi na usalama nk.
chanzo: zanzibar24.

Comments