Serikali ya Ujerumani imetiliana saini na SMZ.

Serikali ya Ujerumani  imetiliana  saini  na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar mkataba wa utengenezaji wa ujenzi mpya wa majumba ya mjerumani kikwajuni  mjini Zanzibar  ili kuziendeleza nyumba hizo kuwa katika  mazingira bora  ya kuishi.


Akizungumza katika hafla hiyo  ya utiaji saini Mstahiki meya wa Mji wa Potsdam Ujerumani Jann Jakobs amesema uimarishajwi wa nyumba hizo  ni muendelezo wa uhusiano mwema uliopo  kati ya Zanzibar  na ujerumani katika  kuwaletea wananchi   maendeleo.

Hata hivyo amesema  mbali na ujenzi wa nyumba hizo  lakini  pia Ujerumani imekusudia kusaidia Zanzibar katika sekta  za maendeleo ikiwemo sekta ya   Elimu, Afya  katika kitengo cha Kensa na mazingira.

Kwaupande wake Mstahiki meya wa Zanzibar Khatib Abrahmani Khatib amesema uhusiano huo  utaweza kuinua  fursa za kiuchumi kati ya  Manispaa ya mji wa Zanzibar na jiji la Potsdam Ujerumani ili  kuweza kunufaika na miradi  mbalimbali ya maendeleo.

Aidha Mstahiki  huyo amesema   ili  kudumisha  ushirikiano  uliopo  wataandaa mikakati ya pamoja  ili  kurahisisha mawasiliano kati yao na uhamasishaji wa vikundi vya vijana kushiriki katika ujenzi huo kupata ajira.

chanzo:zanzibar24.

Comments