New york yajipanga kuinua Sayansi na Teknolojia Zanzibar.

Image result for zanzibarTaasisi  ya  Maendeleo  inayosaidia watoto wakike katika masomo ya sayansi na teknolojia Afrika Malaika  iliyopo New yok imesema  imekusudia   kuwasaidia watoto wa kike  kuwainua kimaendele kutokana na kuwachwa nyuma kimaendeleo  hasa katika mambo ya teknolojia na mambo ya sayansi.

Akizungumza na Zanzibar24 nje ya mafunzo kwa wanafunzi mbalimbali Unguja na Pemba  yaliyofanyika katika uwanja wa baraza  la wawakilishi la zamani kikwajuni Mwenyekiti  wa taasisi ya Afrika Malaika Fiona Barretto amesema  watoto wa kike bado wapo nyuma kujifunza katika masomo ya sayansi  na teknolojia jambo linalochangia  kuonekana  hawana uwezo  na  kushindwa  kupewa  nafasi hasa katika  uongozi.


Hata  hivyo  amesema   endepo wasichana   wakizembea  kutumia fursa hizo   za kujifunza  hawata songa mbele  kimaendelo  lengo la mafunzo hayo ni kumpa kipaumbe  msichana  kujifunza masuala ya sayansi na teknolojia ili kwenda sambamba na hali ya maisha na uchumi wa viwanda.

Kwaupande wake Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Riziki Pembe Juma Akizungumza na Zenji  fm radio mara baada ya kutembelea na kukagua  mafunzo hayo amesema ujio wa taasisi hiyo nifaraja kubwa kwa  walimu na wanafunzi kwani  mafunzo hayo yatamjenga mwanafunzi wa kike  kuwa na moyo wa kusoma masomo ya sayansi ili kufikia malengo.

Aidha Pembe ametoa wito kwa wanafunzi hasa wakike kusoma zaid masomo ya sayansi ili  kupata ujuzi wa kutosha utakaowasaidia  baadae katika maendelo yao.

Zaidi ya wanafunzi mia 400 wamepatiwa mafunzo ya hesababi , sayanasi na teknolojia  pamoja na Kingereza.
Chanzo: Zanzibar24

Comments