
Akitoa tamko la chama kwa waandishi wa habari la kukemea na
kulaani vitendo hivyo Mwenyekiti Mkoa wa mjini Magharibi ambae pia ni
Mbunge viti maalum Maryam Salum Msabaha
amesema vitendo vya ukatili
na udhalilishaji pamoja na vitisho wanavyofanyiwa viongozi wa chama
chao ni viashirio vibaya katika chama na kufanya hivyo ni kutaka
kuikandamiza siasa na kuizoofisha demokrasia.
Akizungumzia mauwaji ya raia pamoja na askari wa jeshi la polisi
katika mkoa wa pwani Kibiti,Rufiji amesema wanalaani vikali na
kulitaka jeshi la polisi kuongeza juhudi za kuwasaka wahalifu ili
kukomesha kabisa vitendo hivyo na kutoa wito kwa wanasiasa
kuwacha tabia za kuingilia kazi za jeshi hilo katika mapambano hayo
ambapo amedaini kufanya hivyo ni kurudiasha nyuma jitihada za
polisi kuwakamata wahalifu hao.
Kwaupande wake Mwenyekiti kanda ya Unguja Said Mzee Said
akizungumzia kauli iliyotolewa hivi karibuni na Rais wa Jamuhuri ya
muungano Tanzania John Pombe Magufuli amesema chama hakikuridhia kauli
hiyo ya kumsitisha mtoto wa kike aliepata ujauzito kwenda shule ni
kumnyima fursa na haki yake ya msingi mtoto wa kike ya kupata elimu.

NA:AMINA ZANZIBAR24
Comments