
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Songwe, Mathias Nyange alimuita mbunge huyo
na kumhoji kutokana na bendera hizo kupeperushwa kwa wingi wakati
Waziri Mkuu Kassim Majaliwa anatarajiwa kuwasili katika eneo hilo ili
kuzungumza na wananchi kwenye mkutano wa hadhara.
Pascal Haonga amesema kuwa alipigiwa simu na kamanda huyo na kutaka
waonane Ikulu ndogo ya Mkoa wa Songwe baada ya kuonana walifikia
makubaliano ya kutoondoa bendera hizo.
“Miongoni mwa mambo tuliyozungumza ni pamoja na
kupandishwa kwa bendera za CHADEMA, katika Mji wa Mlowo, mazungumzo
yameisha na hakuna bendera zitakazoshushwa,” alisema Haonga.
chanzo: zanzibar24.
Comments