Afariki baada ya kuzama kweye shimo lenye maji Unguja.

Related imageMtu mmoja mwanye umri wa maika 18 amefariki dunia baada ya kuzama kweye shimo lenye maji.

Tukio hilo limetokea jana majira ya saa 8 mchana huko Kiwambamvua wilaya ya Kaskazini B, mkoa wa Kaskazini Unguja.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo Sheha wa shehiya ya Kiwambamvua Moh’d  Ali  Ame amesema kijana huyo amezama kwa muda mrefu hadi wao kufikiwa na taarifa hiyo na baada ya kuzipata taarifa hizo aliripoti kwa Mkuu wa wilaya na vikosi vya Polisi ili kushirikiana kumuokoa kijana huyo.


Nae Kamanda wa polisi mkoa wa kaskazini Unguja bi Asya Ramadhan Tawfiq amesema marehemu anajulikana kwa jina la Haji Pandu Faki mkaazi wa Kiwambamvua.

Bi Asya amesema kabla ya kifo chake marehemu alikuwa na wenzake wakaenda sehemu hiyo kwaajili ya kukoga ndipo maji yalipo mzidi na kusababisha kifo chake.

Mwili wa marehemu ulipelekwa Hospitali kuu ya Mnazi mmoja  kwaajili ya uchunguzi na kukabidhiwa jamaa zake kwa ajili ya Mazishi.
chanzo: zanzibar24.

Comments