24 waaga Dunia kwa shambulio la Bomu Kabul.

Watu 24 wameuawa na takriban watu 42 wamejeruhiwa kupelekea na kusababishwa kwa shambulizi la Bomu kwenye mji mkuu wa Afghanistan Kabul.

Imebainika kuwa mshambuliaji wa kujitoa mhanga alijilipua katika eneo lenye washia wengi magharibi mwa mji, Lengo la shambulizi hilo halikutajwa mara moja na hakuna mtu aliyedai kuhusika.


Shambulizi hilo llitokea karibu na nyumba ya afisa wa cheo cha juu serikalini, Mohammad Mohaqiq.

Mashambulizi ya awali yamedaiwa kutekelezwa na Taliban au kundi la Islamic State, Kabul umekumbwa na misururu ya mashambulizi likiwemo lililowaua watu 90 wakati lori lililipuka mwezi Mei.

chanzo: zanzibar24.

Comments