Zanzibar vinakabiliwa na mabadiliko ya tabia ya nchi
yatayosababisha upoteaji wa misitu ya asili, kuongezeka kwa maradhi ya
miripuko na kupotea kwa rasilimali ya mchanga.
Akizungumza na Waandishi wa habari ikiwa ni shamrashamra ya
kuadhimisha Siku ya mazingira duniani ambayo inatarajiwa kuadhimisha
tarehe 5 huko Musoma Butiama Mwenyekiti wa Jumuiya hiyo Amina Yussuf
Kashoro amesema uharibifu wa mazingira unapelekea kuongeza kasi ya
athari za mabadiliko ya tabia ya nchi ikiwemo uchimbaji mchanga,
ukataji
misitu kwa matumizi ya mkaa na kuni, uharibifu wa vyanzo vya maji
ikiwemo ujenzi na ulimaji katika maeneo ya vyanzo vya maji na
kusababisha mafuriko.
Hata hivyo Amina amesema licha yajuhudi mbalimbali zinazochukuliwa
kupambana na matatizo lakini bado yanashika kasi na kuhatarisha
mustakabali wa zanzibar kimazingira hivyo niwakati muafaka kwa jamii
kuwa na uelewa juu ya tatizo hilo na kutafuta njia bora za kilimo na
ufugaji kwani mabadiliko hayo yameathiri sana mifumo ya maisha ikiwemo
kilimo,ufugaji,nishati,utalii pamoja na afya.
Aidha Zacca imeishauri Wizara ya fedha kutenga fedha zaidi kusaidi
miradi ya jamii ya kuhimili athari za mabadiliko ya tabianchi ili
kupunguza kasi kwa jamii kuharibu mazingira kama ukataji miti ovyoo
kwaajili ya mahitaji yao.
Amesema ipo haja serikali kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo
kuweka nguvu zao katika kuwaelimisha jamii juu ya athari hizo kwani
tafiti zilizofavywa na idara ya misitu na maliasili zisizorejesheka
inaonesha zanizbar inapoteza hekta 500 kwa kila mwaka kutokana
wananchi wa Zanzibar wanategemea kuni na mkaa kwa asilimia 97.
chanzo: Zanzibar24
Comments