Wizara ya Elimu Zanzibar yaifunga Skuli ya Laureate baada ya kifo cha Mwanafunzi.

wizara ya elimuWizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali imeifunga Skuli ya Laureate International iliyopo Ole Kianga Mkoa wa Kusini Pemba, kutokana na tukio la kufariki Mwanafunzi wa Darasa la nne aliyepewa adhabu na Mwalimu wa Skuli hiyo.

Akizungumza baada ya kuitembelea Skuli hiyo na kusikiliza maelezo kutoka kwa walimu, Waziri wa Wizara hiyo Mhe. Riziki Pembe Juma amelaani vikali kitendo hicho, amesema Mwanafunzi huyo mwenye umri wa miaka 11 amefanyiwa ukatili mkubwa kwa kupewa adhabu isiyoendana na umri wake.


Nae Waziri wa kazi, uwezeshaji, wazee, vijana, wanawake na watoto Mhe. Maudline Cyrus Castico amesema kitendo alichokifanya Mwalim huyo kwa kumpiga na kumuumiza marehemu ni udhalilishaji na kuvitaka vyombo husika kuchukua hatua za kisheria dhidi yake.

Kwa upande wake Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kusini Pemba Sheikhan Mohammed Sheikhan amesema tayari jalada la kesi hiyo limeshafunguliwa ingawa upelelezi bado haujakamilika.
chanzo: zanzibar24.

Comments