Wizara ya afya yalilia majengo ya hospitali yaliyochakaa Zanzibar.

baraza-la-wawakilishiWizara ya Afya Zanzibar imesema licha kupiga hatua juu ya kutoa huduma kwa wagonjwa lakini wamekabiliwa na matatizo mbalimbali ikiwemo uchakavu wa baadhi ya majengo pamoja na miundo mbinu ya mfumo wa maji taka.

Akiwasilisha hutuba ya makadirio ya Mapato na matumizi ya Fedha ya mwaka 2017/18 katika kikao cha Baraza la wawakilishi chukwani Nje kidogo ya mji wa Zanzibar ,Waziri wa Afya Mahmod thabit Kombo amesema yapo  majengo makuu matatu ambayo ni chakavu kutokana na kutumika kwa muda mrefu.


Amesema miongoni mwa majengo hayo ni pamoja na jengo la hospitali ya Mnazi mmoja ambalo limedumu kwa miaka 94 tangu kuanzishwa kwake,Jengo la hospital ya magonjwa ya akili lililodumu kwa kipindi cha miaka 68 pamoja na kuchakaa kwa Paa la Hospitali ya chakechake.

Aidha amesema mbali na tatizo hilo wizara ya afya imekabiliwa na tatizo la kuengezeka kwa mahitaji ya huduma za afya wanazohitaji kupatiwa wagonjwa licha ya kutengewa bajeti na serikali.

Akizungumzia suala la kupandisha hadhi hospitali Kuu ya Mnazi mmoja Waziri kombo amesema  katika mwaka 2017/18 wizara imekusudia kuengeza upatikanaji wa vifaa tiba ,kuendeleza ujenzi wa wodi mpya ya watoto inayotarajiwa kuwa na vitanda100 pamoja na kulikarabati jengo la macho lililopo katika hospital hiyo ili kutowa huduma bora kwa wagonjwa.

Hata hivyo amesema wizara pia imenunua mashine itanayowasaidia wagonjwa wa matatizo ya figo (dialysis ) kuweza kusafisha damu, pamoja na kuimarisha huduma za uchunguzi ikiwemo huduma za X-RAY, MRI na ULTRASOUND.
chanzo: Zanzibar24.

Comments