Utafiti uliofanywa na Taasisi ya
taifa ya Kujua kusoma na Kuandika nchini Uingereza umeonesha kuwa
theluthi moja ya wavulana nchini humo wanasema wanafurahia kusoma
vitabu.
Taasisi hiyo imegundua kushuka kupenda kusoma vitabu kwa wavulana kati ya umri wa miaka minane mpaka 16.
Asilimia
72 ya wavulana wenye umri kati ya miaka minane mpaka 11, waliohojiwa
walionesha kupenda kusoma, lakini asilimia hiyo imeshuka mpaka kufikia
asilimia 36 wanapofika umri wa miaka 14 mpaka 16.
Wasichana
waliohojiwa kati ya umri wa miaka minane mpaka 11, asilimia 83 walikuwa
wakifurahia kusoma vitabu, lakini asilimia hiyo ilishuka mpaka 53 kwa
wasichana wa umri wa miaka 14 mpaka 16.
Mkurugenzi wa taasisi hiyo
Jonathan Douglas mapenzi ya vijana kupenda kusoma vitabu yamekuwa
yakipungua kwa kasi baada ya kumaliza shule.
chanzo:Bbc.

Comments