Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi waitaka SMZ kuwa makini wakati wa kufunga mikataba.

baraza-la-wawakilishiWajumbe wa Baraza la Wawakilishi wameitaka serikali ya Mapinduzi  kuwa makini wakati wa kufunga mikataba ya ujenzi wa majumba  na wakandarasi  ili kuepusha hasara kwa serikali na kuepukana na  majengo yasiyokuwa na viwango na ubora ambayo yanaweza kuhatarisha maisha ya wananchi.

Wakizungumza katika Kikao cha baraza la Wawakilishi Ali Salum Haji,Miraji Khamis Kwanza na Sheha Hamad Matar
wamesme  kutokana na matatizo na kasoro mbalimbali zilizojitokeza kutokana majengo yasiyo na viwango  yaliyojengwa na wakandarasi  ni mabovu licha ya serikali kutoa  mabillion ya Fedha  yameweza kusababisha  hasara yakiwemo majengo ya skuli kuvuja, majengo ya wizara pamoja na nyumba za viongozi pamoja na nyumba za maendeleo wanazoishi wananchi maeneo mbalimbali.

Naye Mwanasheria Mkuu wa Serikali Said Hassan Said amesema Serikali imekuwa inaingia katika mikataba ya ujenzi kwa wakandarasi ambao wanafani na kazi hiyo kwa mujibu wa sheria na sifa za kuingia kwenye mkataba   lakini chanzo cha majengo hayo kutokuwa na ubora  na viwango ni usimamizi mbovu wa  mikataba hiyo  pamoja na watendaji wa serikali  kutokuwa na udhati wa kufatilia shughuli za serikali.

Kwaupande wake Naibu Waziri wa wizara hiyo Mohammed Ahmada  Salum amesema katika mwaka wa Fedha 2017/2018  serikali itahakikisha kuyafanyika kazi matatizo yote yaliyojitokeza ili yasijirejee tena kutokana na hasara kubwa ilopatikana kwani majengo mengi ni mabovu hivi sasa ili kuhakikisha  mikataba inayofungwa na serikali na wakandarasi inasimamiwa ipasavyo.

chanzo: Zanzibar24

Comments